TANZANIA COMMISSION FOR SCIENCE AND TECHNOLOGY
(COSTECH)

News

COSTECH WASHIRIKIANA NA SWEDEN,SIDO KUZINDUA KITABU CHA KONGANO BUNIFU

TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa ushirikiano na watu wa Swedeni na Shirika la Viwanda vidogo, SIDO wamezindua kitabu cha kongano bunifu ambacho kinalenga zaidi kuwasaidia wabunifu na watafiti katika kufanikisha zaidi bunifu na bidhaa zao sokoni.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH)Dkt. Amosi Nungu amesema wamezindua kitabu ambacho kinaongelea maswala ya kongano bunifu, wakishirikiana na wenzao kutoka Swedeni na Sido.