
COSTECH YAWASILISHA TAARIFA YA UTEKELEZAJI MRADI WA HEET
Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) ni miongoni mwa wanufaika wa Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Elimu ya Juu (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia ukijumuisha utekelezaji toka Vyuo Vikuu 19 na Taasisi 3 ambapo umetoa ufadhili wa fedha za mradi huo.
COSTECH ni miongoni wa Taasisi wanufaika wa mradi wa 'HEET' ukitekeleza kupitia nyanja ya kutafsiri matokeo ya utafiti kufikia hatua ya bidhaa kwa ajili ya kubiasharishwa.
Aidha, Taasisi wanufaika wa mradi kupitia Benki ya Dunia imeweka utaratibu wa kuendesha mikutano ya pamoja na wanufaika wa ufadhili huo kila baada ya miezi sita (6) ili kutathimini Maendeleo ya utekelezaji wa malengo ya mradi kwa kila Chuo na Taasisi, Benki ya Dunia inaendesha mkutano wa tatu (3) toka mradi huo uanze utekelezaji wake.