Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia COSTECH imeendesha Mdahalo kati ya wadau wa Viwanda na Vyuo Vikuu ili kujadili kwa pamoja changamoto zinazojitokeza katika eneo la mahusiano ili kuboresha mitaala ya elimu na kujadili njia za kutatua changamoto na kuongeza kuongeza tija na ufanisi pamoja na kasi ya uzalishaji wa ukuaji wa sekta ya viwanda nchini.
Mdahalo huo ulifunguliwa na Prof. Maulid Mwatawala Mwakilishi wa Makamu wa Chuo cha Kilimo SUA, kwa kuwakaribisha wadau wote na amewataka kuhakikisha wanaweka mikakati bora ya mahusiano ya pamoja ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiuchumi kwa kuangalia urasmishaji na uhawilishaji wa Teknolojia kwa mandeleo ya viwanda nchini. Vilevile kuangalia teknolojia zinazoakisi mazingira halisia ya nchi katika kuongeza ushindani wa soko la ajira na umahiri wa wanafunzi/wahitimu kukidhi mahitaji ya ukuaji wa sekta ya viwanda nchini.
Wadau mbalimbali waliojitokeza wakati wa ufunguzi wa mdahalo huo na kuwasilisha mada mbalimbali na kujadili changamoto kwa pamoja ni kutoka Vyuo Vikuu nchini kikiwepo Chuo Kikuu Cha Kilimo SUA, kupitia (DPRTC) ambayo ni Kurugenzi ya Uzamili, Utafiti, Uhawawilishaji wa Teknolojia na Ushauri wa Kitaalamu kupitia Kitengo cha “SUA Innovation Hub” na Chuo Kikuu Cha Mtakatifu Joseph- SJUIT kupitia idara ya ITAF, Taasisi ya Teknolojia ya Dar es salaam (DIT) na wadau wa Kongano (Cluster) ya Mkoa wa Morogoro wanaofahamika kwa jina “Morogoro Food Processors Clusters Initiative”
Aidha, wawakilishi kutoka Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) inayosimamia Sera na Ushawishi wa viwanda anaeleza ni muhimu kufanya tathimini ya mahitaji “Training Need Assessment” ili kusaidia walimu na wanafunzi kuendana na mazingira halisi. Kuahidi kuendelea kushirikiana na COSTECH kama mshauri kwa kuwa kazi yao inategemea utafiti (Evidence based) kuendesha shughuli zao. Pia Taasisi ya wafanyabiashara wenye Viwanda, Biashara na Wakulima (TCCIA) amesema wanaendeleza mahusiano na Vyuo vikuu na viwanda kwa lengo la kuwaunganisha ili kuwapatia mafunzo kwa vitendo au uhalisia kwa kusudi la kukuza kada zao na uzoefu wa ujasiriamali katika soko la ushindani la ndani na nje ya nchi.
Akifunga Mdahalo huu Dkt. Athumani Mgumia, Kaimu Mkurugenzi wa Kituo cha Uhawishaji wa Teknolojia (CDTT) ambae pia ni muwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH amewashukuru wadau kwa kujitokeza na kujadili kwa pamoja changamoto mbalimbali zinazojitokeza na amekaribisha mawazo yanayolenga kufanya maboresho na kutoa mchango chanya kwa maendeleo endelevu ya viwanda nchini.
Mdahalo huu umeandaliwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa ndani na nje ya Taasisi.
Picha ya Pamoja ya Washiriki wa Mdahalo wa Ubunifu na uboreshaji wa mahusiano kati ya Vyuo vikuu na wadau wa Viwanda nchini. Siku ya Jumatano 17, Juni 2020. Chuo Kikuu kilimo SUA, Mkoa wa Morogoro.
IMEANDALIWA NA;
AFISA UHUSIANO
TUME YA TAIFA YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA (COSTECH)